skip to main |
skip to sidebar
Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) imehamasisha jumuiya ya
wafanyabiashara nchini kuchangamkia fursa za biashara katika Umoja wa
Mataifa (UN).
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa TPSF, Godfrey
Simbeye, katika semina ya kuwahamasisha wafanyabiashara wa Tanzania
kufahamu na kuzitumia fursa za biashara zinazojitokeza UN.
Semina hiyo iliyofanyika jijini Dar es Salaam hivi karibuni
ilitayarishwa na TPSF kwa kushirikiana na kitengo cha manunuzi cha ofisi
ya UN. semina hiyo ililenga kuwahamasisha wafanyabiashara, ili waweze
kuwekeza kimataifa na kutanua wigo wa biashara.
Simbeye alisema kuwa
“Tumeleta wafanyabiashara wa Tanzania katika semina hii, ili kuweza
kuangalia ni fursa zipi wanazoweza kuzipata katika zabuni za Umoja wa
Mataifa,”
Aliongezea kuwa Tanzania inashiriki kwa kiwango kidogo katika
zabuni za UN, kitu ambacho kinawashangaza wadau mbalimbali hasa kutokana
na mchango mkubwa wa Tanzania katika kuleta amani kwenye nchi nyingi
duniani.
“Hatujafanya semina ya namna hii kwa miaka tisa sasa, kama
inavyofanywa na nchi jirani kama Kenya na Uganda… kuna fursa nyingi za
biashara na Umoja wa Mataifa,” alisema Simbeye.
Mkuu wa Idara ya Manunuzi UN, Yavar Khan, alisema kuna kila
sababu kwa Watanzania kushiriki kwa kiwango kikubwa katika kufanya
biashara na umoja huo.
Ofisa Manunuzi Mwandamizi wa Ujumbe wa UN
Sudan ya Kusini (UNMISS), Bruno Maboja, alisema mategemeo yao ni kuona
kampuni za Tanzania zinashiriki katika biashara na umoja huo.
0 comments:
Post a Comment