skip to main |
skip to sidebar
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za
Serikali (CAG), Ludovick Utouh (katikati) akizungumza kwenye mkutano na
waandishi wa habari uliofanyika bungeni, mjini Dodoma juzi. Kushoto ni
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Zitto Kabwe
na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (Laac),
Rajab Mbarouk Mohammed
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa
Hesabu za Serikali (CAG), amezinyooshea kidole mamlaka mbili za Serikali
kwa kushindwa kudhibiti uingizaji wa bidhaa zisizo na ubora nchini.
CAG
imetoa taarifa kuhusu ukaguzi wa ufanisi na ukaguzi maalumu kwa kipindi
kinachoishia Machi 31, 2014, imezitaja taasisi hizo kuwa ni Shirika la
Viwango Tanzania (TBS) na Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA),
akisema zilipwaya katika ukaguzi wa ubora wa chakula kinachoingizwa na
kuzalishwa nchini.
Taarifa hiyo imebainisha kuwa ufuatiliaji ulishindwa kuzuia viwanda vya usindikaji chakula kuvunja sheria mara kwa mara.
Asilimia
80 ya viwanda vilivyokuwa vimekiuka sheria havikuchukuliwa hatua, huku
kukiwapo makosa ya kujirudiarudia kwa wasindikaji na waagizaji chakula
nje ya nchi. Kwa mujibu wa CAG.
Taarifa hiyo imesema kwa hali
inavyoonekana, idadi ya bidhaa hafifu nchini imekuwa ikiongezeka kwa
miaka mitatu kwa kati ya asilimia 30 na 40 kutoka mwaka wa fedha wa
2010/2011.
Bidhaa hizo nyingi hupita katika bandari na mipaka ya
Tanzania ambayo wakaguzi wa TBS walitakiwa kuzikagua, lakini kutokana na
upungufu wa ukaguzi, zimekuwa zikiingia nchini.
Taarifa hiyo,
CAG alisema ukaguzi wa ubora wa bidhaa zinazoingia nchini haukufanyika
vizuri na vya kutosha na ukaguzi wa bidhaa kutoka nje haukufanywa kwa
kuzingatia viashiria hatarishi.
“Bidhaa zote zilipewa kipaumbele
sawa wakati wa ukaguzi licha ya ukweli kwamba baadhi ya bidhaa
zinajulikana kuwa na athari kubwa kwa afya na mazingira ya walaji
nchini,” asema
0 comments:
Post a Comment