skip to main |
skip to sidebar
Dodoma. Mbumge wa Chwaka (CCM) , Yahaya Kassim Issa ameitaka Serikali kuchukua hatua ya kukomesha uzinzi ili kuzuia maambukizi mapya ya ugonjwa ukimwili.
Alisema hayo jana wakati akichangia hotuba ya bajeti ofisi ya waziri Mkuu kwa mwaka wa fedha 2014/2015.
Suala la kwamba tunawapa watu dawa. mtu mmoja anaonekana kuwa imara(strong) anaambukiza wengine haitusaidii, alisema.
Alipohoji kuwa iwapo kila mtu kati ya watu zaidi ya milioni moja ambao wanaishi na virusi vya ukimwi(VVU) ataambukiza mmoja, kutakuwa na watu wangapi wanaoishi na virusi hivyo? Na watu hawa unadhani unawapa dawa, kwa kweli hatuwezi kufanikiwa lazima mtumie uhalisia wa kupambana na tatizo hili, alisema.
0 comments:
Post a Comment