Friday, May 9, 2014

DERAVA AFARIKI AKIFANYA MAPENZI GEST.

Kifo cha dereva  kimezusha  gumzo miongoni mwa wakazi  wa mkoa wa SINGIDA  na Vitongoji  vyake.

Singida : Dereva  wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba mkoani singinda, Juma  Juma(52) ,amefariki dunia wakati akifanya mapenzi kwenye nyumba ya kulala wageni akiwa na mwanamke ambaye imedaiwa ni mhudumu wa baa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Geofrey  Kamwela alisema  tukio  hilo lilitokea Mei 3, saa 4:00 usiku chumba kwenye Na. S.2 cha nyumba ya kulala  wageni ijulikanayo  kwa jina la Top Life New mjini Kiomboi.

Alisema  saa 6:00 usiku siku ya tukio hilo, dereva  huyo alimuaga mpangaji wake kuwa anatoka mara moja na asingechelewa kurudi nyumbani kwa hiyo usifunge mlango wa mbele wa nyumba.

Alisema kuwa saa  mbili baadaye , dereva huyo alionekana akiwa baa iliyoko  kwenye nyumba hiyo ya kulala wageni ambayo iko mita  50  kutoka nyumbani  kwema.

"Muda huo Juma alionekana akiwa na mmoja wa wahudumu wa baa hiyo aitwaye Agness Mayo (32) anayesadikiwa kuwa na uhusiano naye wa kimapenzi ," alisema.

Kamwela alisema mhudumu  huyo wa baa alitoweka Mei 4 , mwaka huu  baada ya kuaga kwamba anakwenda kanisani na kutorokea kusikojulikana.

Hata hivyo , ufunguo wa chumba alicholala Juma zilikutwa chumba cha kulala wahudumu wenzake.

Kamanda huyo alisema kuwa tangu siku Mei 3, chumba alicholala Juma hakikufunguliwa hadi Mei 5 mwaka huu wakati mwili wa dereva huyo ulipokutwa ukiwa umeharibika.

"Uchunguzi zaidi wa tukio hilo unaendelea ikiwa ni pamoja na kutafuta mhudumu aliyetoroka ili ahojiwe na kisha kufikishwa mahakamani endapo atabainika kuhusika na tukio," alisema kamanda Kamela.


chanzo cha habri : Mwananchi (Mei 9,2014)

0 comments:

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More

 
Design by Free WordPress Themes | Bloggerized by Lasantha - Premium Blogger Themes | Powerade Coupons