skip to main |
skip to sidebar

MBU Aedes au Aedes aegypti ni wadudu wenye mabawa mawili na miguu sita kutoka familia ya Culicidae.
Mbu
huyo asili yake ni Afrika lakini hivi sasa amesambaa sehemu mbalimbali
duniani hasa sehemu za tropiko na anapatikana majira yote ya mwaka hasa
sehemu zenye maji maji. Machapisho mbalimbali ya kimataifa ya utafiti wa
kisayansi kuhusu mbu huyo yanaeleza kuwa amekuwepo kwa zaidi ya miaka
milioni 150 iliyopita na kusabisha maradhi kwa binadamu wa kale.
Utafiti
wa awali uliofanywa na mwanasayansi Fredric Hasselquist mwaka 1757
ulitaja mbu huyo kwa jina la Culex aegypti. Jina la Aedes aegypti
lilianza kutumika mwaka 1920 na lilianzishwa na mwanasayansi Harrison
Gray Dyar, Jr. Aedes ni mbu anayeeneza virusi vinavyosababisha ugonjwa
maarufu kwa jina na chikungunya, homa ya manjano na homa ya dengue
ambayo hivi sasa inaenea kwa kasi katika jiji la Dar es Salaam.
Mbu
Aedes ni miongoni mwa wadudu walioko katika hali ya metamofisisi ambao
maisha yao hupitia hatua nne zinazowafanya kuwa na tabia na maumbo
tofauti ambazo ni yai, lava, pupa na mbu kamili. Unaweza kumtambua mbu
huyo kwa kuwa ana mistari meupe miguuni.
Tofauti na mbu
wanaoeneza ugonjwa wa malaria ambao huuma usiku, mbu wa homa ya dengue
huuma mchana na usiku.Taarifa za kisayansi zinaeleza kuwa mbu jike ndiye
hasa anayeuma na kueneza kirusi cha homa ya dengue wakati akifyonza
damu katika mwili wa binadamu.
Mbu jike hutumia damu kama lishe
kuu ili aweze kurutubisha mayai yake ili kuendeleza kizazi cha mbu hao.
Baada ya kunyonya damu ya kutosha mbu jike huweza kutaga mayai 100 hadi
200 kwa uzao mmoja. Jike anaweza kutaga mara tano katika kipindi cha
uhai wake.
Mbu aliyepevuka huishi kwa wastani wa wiki mbili hadi
mwenzi moja hivyo mbu mmoja aweza kutaga mayai kati ya 500 hadi 1,000
kwa kipindi cha wiki mbili hadi mwenzi mmoja. Wingi wa mayai unategemea
kiasi cha damu aliyopata kwa kuwa kadiri anavyopata damu nyingi ndivyo
anavyotaga mayai mengi zaidi.
Ingawa mbu huyo anataga mayai 200
katika uzao mmoja, hutaga mayai sehemu tofauti ili kuzuia kizazi chache
kisiangamie kwa urahisi endapo adui atavamia mayai hayo. Mayai ya mbu
aina ya Aedes yana umbo la mviringo uliochongoka, yana gamba laini na
urefu wa milimita moja. Mbu anapotaga hutoa mayai meupe ila baada ya
dakika chache hubadilika na kuwa na rangi nyeusi.
Mbu hawa
hupendelea kuzaliana kwenye maji yaliyotuama karibu na makazi ya watu au
hata ndani ya nyumba. Mbu huyo anataga kwenye madimbwi ya maji hasa
sehemu yenye mafuriko, kwenye mapango ya miti, sehemu zenye mashimo au
mapango yaliyotengenezwa na binadamu.
Pia wanataga mayai hao
kwenye mapipa, vyungu na makopo ya maua, kweye chupa na makopo
yaliyotupwa ovyo, matairi ya gari, vifuu vya nazi, matambara katika
viambaza vya nyumba na sehemu zozote zile zenye upenyo hasa katika lundo
la uchafu katika viambaza vya nyumba.
Mayai hayo huanguliwa kwa
siku tofauti kulingana na hali ya hewa na mazingira ya eneo husika.
Sehemu yenye joto kama Dar es Salaam mayai huanguliwa katika siku mbili
tu lakini sehemu zenye baridi mayao huchukua hadi siku saba kabla ya
kuanguliwa. Mayai ya mbu wa homa ya dengue hayaanguliwi yote kwa wakati
mmoja, wakati wa kuanguliwa yanaweza kupishana saa chache au siku nzima
kulingana na mazingira ya eneo husika.
Kupishana huko huwezesha
kizazi cha mbu kuwepo wakati wote katika majira ya mwaka ikiwa eneo
husika litakuwa na hali ya maji maji. Mayai ya mbu anayeeneza ugonjwa wa
dengue yanauwezo wa kuhimili hali ya hewa na kukaa muda mrefu bila
kuharibika. Ikiwa mayai hayo yametagwa wakati wa kiangazi yanaweza kukaa
zaidi ya mwaka mzima bila kuanguliwa kisha huanguliwa kipindi cha mvua
ili kiluilui waweza kuishi na kukua vyema.
Kitendo cha yai kukaa
muda mrefu kinasababisha changamoto katika harakati za kumuangamiza mbu
huyo mwenye uwezo wa kudhuru na hata kuua binadamu ili waweze kuendeleza
kizazi chake. Baada ya mayai kuanguliwa viluwiluwi vya mbu huishi kwa
kula chembechembe zinazopatikana kwenye maji.
Baadhi ya
chembechembe ni ndogo sana haziwezi kuonekana kwa macho bila msaada wa
darubini. Viluwiluwi hao huogelea kwenye maji na wakati mwingine huja
juu ya maji. Wanaweza kuishi kwenye kina kifupi cha maji ndio maana
wanaweza kuzaliana kwenye makopo ya maua yanayoruhusu maji kutwama,
kwenye vifuu vya nazi na maeneo mengine yanayohifadhi maji kwa muda
mrefu.
Viluwiluwi wanakua kulingana na hali ya hewa, endapo kuna
hali joto anaweza kukua kwa muda mfupi katika siku moja ila kama kuna
hali ya ubaridi na maji ya kutisha anaweza kubaki kwenye maji hata kwa
zaidi ya mwenzi mzima. Lava aliyekomaa huwa na urefu wa milimita nane.
Mbu dume hukua haraka zaidi hivyo hubadilika na kuwa mbu kabla ya mbu
jike.
Hatua ya kukua yaani yai, lava na pupa huchukua muda mrefu
ikilinganishwa na muda ambao pupa anapobadilika na kuwa mbu kamili. Mbu
aliyepevuka anaweza kuishi kwa wastani wa wiki mbili hadi mwezi mzima na
kusababisha maradhi mbalimbali yanayotokana na homa ya dengue.
0 comments:
Post a Comment