Wednesday, May 14, 2014

HANDENI-MWANANKE WA MIAKA 50 AJIFUNGUA KIUMBE CHA AJABU

 Inakuwaje mwanake wa miaka zaidi ya miaka 45 kupata mtoto ikiwa katika masuala ya uzazi inasemekana kuwa mwanamke akifikisha umri wa miaka zaidi ya  45 atakuwa hana uwezo wa kuzaa.


Kisha  Mwanamke mmoja mkazi wa Kata ya Sindeni wilayani ya handeni mkoa Tanga , Mwajuma Seif (50) amejifungua mtoto mwenye umbile la ajabu hali iliyomtisha na kufikia hatua ya kuwaomba madaktari wamfunge kizazi kwa kudai amechoka na anaogopa kubeba mimba zaidi.
Mtoto huyo aliyezaliwa na umbile la ajabu aliweza kuishi kwa siku mbili tu baada kuacha gumzo katika Mji wa Handeni na Mkoa wa Tanga kwa ujumla kutokana na jinsi alivyokuwa.


Mwanamke huyo  hadi sasa bado yupo wodini kutokana na hali yake ya afya kutokuwa imara  Mwajuma Seif  alisema, awali alijua amebeba ujauzito wa kawaida na hakuwa na wazo lolote kuwa inaweza kuwa ni mimba ya mtoto wa ajabu ingawa alishangazwa na uzito wa mimba hiyo na kudhani walikuwa watoto mapacha.

Pia Kaimu Mganga Mkuu na Mganga mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya Handeni, Dk. Bakari Mdoe alisema tumbo la mama huyo liliwatia mashaka na ndipowalipomuweka katika uangalizi maalumu hadi alipofikia muda wa kujifungua.

0 comments:

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More

 
Design by Free WordPress Themes | Bloggerized by Lasantha - Premium Blogger Themes | Powerade Coupons